Random Posts

Spika Ndugai Atembelea Ofisi za Uhamiaji Mei 3, 2018 mjini dodoma.

 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kulia) akisalimiana na Koplo, Yakobo kiwawa (kushoto) wakati akiingia katika Ofisi ya Uhamiaji leo Mjini Dodoma Kwa ajili ya kuchukuliwa alama za vidole ili  kutengenezewa pasi/hati ya kusafiria.
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akisaini kitabu cha wageni walipotembelea Ofisi ya uhamiaji leo Mjini Dodoma kabla ya kuchukuliwa alama za vidole kwa ajili ya kutengenezewa pasi ya kusafiria.
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akichukuliwa alama za vidole kwa ajili ya kutengenezewa pasi ya kusafiria leo katika Ofisi ya uhamiaji Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kulia) akizungumza na Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji Mkoa wa Dodoma, Ndg. Edwin Mwasota (kulia)  katika Ofisi za uhamiaji Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (aliekaa) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa kutoka Ofisi ya uhamiaji leo Mjini Dodoma wakiongozwa na Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji Mkoa wa Dodoma, Ndg. Edwin Mwasota (wa pili kulia waliosimama)
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

Post a Comment

0 Comments